Sunday, 28 August 2016





Katibu Mkuu Msaidizi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia idadi ya watu Natalia Kanem amesema vijana 500 millioni kote duniani (25%) wanaishi katika familia Masikini huku Afrika ikiwa na idadi kubwa zaidi.
Kanem alisema hayo jana katika maadhimisho ya siku ya Vijana Duniani yaliyofanyika katika uwanja wa Zakheim Mbagala na kauli mbiu ikiwa ni “Tokomeza umasikini kwa uzalishaji endelevu na matumizi yenye tija”.
“Watu 2 billioni Duniani kote ni vijana wengi wameshindwa kufanikiwa katika ndoto zao kutokana na changamoto zinazofanana, na kauli mbiu hii inagusa uhalisia unaoweza kuwafikisha katika mafanikio vijana wa Tanzania, Afrika na Dunia nzima”, alisema Kanem.
Kanem aliongeza kuwa vijana ni nguvu kazi na ni mhimu kwa maendeleo ya Taifa hivyo katika safari yao ya kuelekea utu uzima na uzee  sasa ni muda wa kujitathimini wao ni wakina nani, ni zipi haswa ni ndoto zao na kutafta fursa ili waweze kuzifanikisha.
Hata hivyo vijana waliohudhuria walitoa tamko na maombi kwa Serikali ili waweza kuzishinda changamo zinazosababisha kukwama kwa mafanikio yao.
Muwakilishi wa vijana Dickson Goerge alisema Serikali haina budi kuboresha Sekta ya Elimu kwa ujumla wake, Sekta ya Afya, kuweka nafasi za vijana katika uwakilishi wa ngazi za juu, Kupiga vita Rushwa, Kuasimamia kanuni za Utawala Bora, Usimamizi mzuri wa Rasilimali za Taifa na kuwapatia vijana fursa za ajira.
“Vijana tunahitaji mfuko wa Taifa kwaajili ya kutuwezesha katika mambo yetu, tunahitaji usimamizi mzuri wa rasilimali za Taifa hususani mbuga na madini, Uwepo wa fursa za ajira, tunahitaji maboresho katika sekta ya afya kuwe  na bima ya matibabu kwaajili yetu ili sasa tuweze kupambana na umasikini na kuongeza uzalishaji katika Taifa letu”, alisema George.
Mratibu wa progrmu ya kuendeleza  ujasiliamali kwa vijana Noreen Toroka kutoka Shirika la kazi la Umoja wa mataifa (ILO) alisema Serikali ya Tanzania ipo katika mpango wa kuelekea katika nchi ya viwanda lakini vijana ambao ndiyo chachu katika kufanikisha hilo bado wanachangamoto nyingi ikiwa ni pamoja na Ukosefu wa ajira na umasikin.
“Licha ya kwamba ripoti ya hivi karibuni inaonesha kupungua kwa tatizo la ajira kwa asilimia 2 kutoka asilimia 13 mwaka 2006 - aslimia 11 mwaka 2015 bado kuna uhitaji mkubwa kwani ajira kwa vijana inaweza hata kuboresha sekta nyingine ikiwemo ya afya”, alisema Toroka.

Aidha kauli ya Katibu Mkuu wa Umoja wa Matiafa Bam-Ki-Moon kuhusu siku ya vijana mwaka huu inaelezea changamoto ambazo zinakwamisha mafanikio ya vijana kuwa ni Umasikini, Kushindwa kumiliki mali, Njaa, Upotezaji wa Chakula, , kushindwa kunufaika na rasilimali za nchi zao na  uharibifu wa mazingira unatokana na viwanda.
“Ukiwekeza katika vijana wanachangia katika upatikanaji wa masoko mapya, soko huria, makazi endelevu, usafiri endelevu na mengine mengi yanayowanufaisha watu na Dunia kwa ujumla”, alisema Bam Ki-Moon.
Aidha Moon alitoa wito kwa vijana wote Duniani kushiriki kikamilifu katika kufanikisha malengo endelevu ya Dunia kulingana na mahitaji ya Serikali za nchi zao.

No comments:

Post a Comment