Katibu Mkuu Msaidizi wa Shirika la Umoja
wa Mataifa linaloshughulikia idadi ya watu Natalia Kanem amesema vijana 500
millioni kote duniani (25%) wanaishi katika familia Masikini huku Afrika ikiwa
na idadi kubwa zaidi.
Kanem alisema hayo jana katika maadhimisho
ya siku ya Vijana Duniani yaliyofanyika katika uwanja wa Zakheim Mbagala na
kauli mbiu ikiwa ni “Tokomeza umasikini kwa uzalishaji endelevu na matumizi
yenye tija”.
“Watu 2 billioni Duniani kote ni vijana
wengi wameshindwa kufanikiwa katika ndoto zao kutokana na changamoto
zinazofanana, na kauli mbiu hii inagusa uhalisia unaoweza kuwafikisha katika
mafanikio vijana wa Tanzania, Afrika na Dunia nzima”, alisema Kanem.
Kanem aliongeza kuwa vijana ni nguvu kazi
na ni mhimu kwa maendeleo ya Taifa hivyo katika safari yao ya kuelekea utu
uzima na uzee sasa ni muda wa
kujitathimini wao ni wakina nani, ni zipi haswa ni ndoto zao na kutafta fursa
ili waweze kuzifanikisha.
Hata hivyo vijana waliohudhuria walitoa
tamko na maombi kwa Serikali ili waweza kuzishinda changamo zinazosababisha
kukwama kwa mafanikio yao.
Muwakilishi wa vijana Dickson Goerge
alisema Serikali haina budi kuboresha Sekta ya Elimu kwa ujumla wake, Sekta ya
Afya, kuweka nafasi za vijana katika uwakilishi wa ngazi za juu, Kupiga vita
Rushwa, Kuasimamia kanuni za Utawala Bora, Usimamizi mzuri wa Rasilimali za
Taifa na kuwapatia vijana fursa za ajira.
“Vijana tunahitaji mfuko wa Taifa kwaajili
ya kutuwezesha katika mambo yetu, tunahitaji usimamizi mzuri wa rasilimali za
Taifa hususani mbuga na madini, Uwepo wa fursa za ajira, tunahitaji maboresho
katika sekta ya afya kuwe na bima ya
matibabu kwaajili yetu ili sasa tuweze kupambana na umasikini na kuongeza
uzalishaji katika Taifa letu”, alisema George.
Mratibu wa progrmu ya kuendeleza ujasiliamali kwa vijana Noreen Toroka kutoka
Shirika la kazi la Umoja wa mataifa (ILO) alisema Serikali ya Tanzania ipo
katika mpango wa kuelekea katika nchi ya viwanda lakini vijana ambao ndiyo
chachu katika kufanikisha hilo bado wanachangamoto nyingi ikiwa ni pamoja na
Ukosefu wa ajira na umasikin.
“Licha ya kwamba ripoti ya hivi karibuni
inaonesha kupungua kwa tatizo la ajira kwa asilimia 2 kutoka asilimia 13 mwaka
2006 - aslimia 11 mwaka 2015 bado kuna uhitaji mkubwa kwani ajira kwa vijana
inaweza hata kuboresha sekta nyingine ikiwemo ya afya”, alisema Toroka.
Aidha kauli ya Katibu Mkuu wa Umoja wa
Matiafa Bam-Ki-Moon kuhusu siku ya vijana mwaka huu inaelezea changamoto ambazo
zinakwamisha mafanikio ya vijana kuwa ni Umasikini, Kushindwa kumiliki mali,
Njaa, Upotezaji wa Chakula, , kushindwa kunufaika na rasilimali za nchi zao
na uharibifu wa mazingira unatokana na
viwanda.
“Ukiwekeza katika vijana wanachangia
katika upatikanaji wa masoko mapya, soko huria, makazi endelevu, usafiri
endelevu na mengine mengi yanayowanufaisha watu na Dunia kwa ujumla”, alisema
Bam Ki-Moon.
Aidha Moon alitoa wito
kwa vijana wote Duniani kushiriki kikamilifu katika kufanikisha malengo
endelevu ya Dunia kulingana na mahitaji ya Serikali za nchi zao.
No comments:
Post a Comment